Dhana ya neno “Tafsiri” imeelezwa na watalamu mbalimbali na kwa nyakati tofauti tofauti kama ifuatavyo:

Kwa mujibu wa (1965:20). Tafsiri ni ni kuchukua mawazo yaliyo katika maandishi kutoka lugha moja (lugha chanzi) na kuweka badala yake mawazo yanayolingana na hayokutoka lugha nyingine (lugha lengwa).

TUKI, (2002). Tafsiri ni kutoa mawazo katika lugha moja kwenda lugha nyingine bila kubadilisha maana.

Mwansoko na wenzake, (2006). Wanafasiri tafsiri kuwa ni zoezi la la uhawilishaji wa mawazo katika maandishi kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine.

Mshindo, (2010) anasema, kufasiri ni kufafanua maana ya matini moja na kutayarisha baadae matini nyingine inayowiana nayo ambayo inawakilisha ujumbe uleule uliokuwa katika matika matini ya awali kwa kutoka lugha nyingine.

Newmark (1992), Tafsiri ni jaribio la kuwasilisha ujumbe uleule ulioandikwa katika lugha moja kwa lugha nyingine.

AS-Safi akimnukuu Dubois (1982) anaeleza kuwa tafsiri ni uelezaji wa mawazo katika nyingine (lugha lengwa) wa kilichoelezwa katika lugha nyingine (lugha chanzi).

Larson (1984)  anaeleza kuwa, Tafsiri inahusisha uhawilishaji wa maana iliyoko katika maandishi katika lugha chanzi kwenda lugha lengwa.

Katika maana zote hizi, tunaona kuwa ndani ya fasili ya tafsiri kuna mambo matatu mhimu ambayo ni:

·         Ujumbe au mawazo yanayotakiwa kutafsiriwa sharti yawe katika maandishi.

·         Mawazo au ujumbe katika lugha chanzi na lugha lengwa sharti yalingane.

·         Tafsiri inaweza kuwa kutoa maana ya maneno au mawazo.

Hivyo, tafsiri ni zoezi la uhawilishaji wa mawazo, ujumbe au taarifa iliyopo katika maandishi kutoka lugha chanzi kwenda lugha lengwa bila kupoteza maana ya msingi na mtindo uliotumika katika matini chanzi.

Wanjala (2011) anaeleza kuwa, historia ni taarifa, maelezo na ucahambuzi wa matukio, watu na nyakati teule zinazoathiri maisha ya wanajamii husika, sasa na siku za usoni. Ujuzi wa historia hutuwezesha kuthibiti na kuthamini misingi na maendeleo ya taaluma zetu. Ufafanuzi wa historia ya tafsiri kidunia, huelezewa kupitia vipindi bainifu vitano vya tajiriba ya binadamu kwa kuegemea maendeleo na utamaduni.vipindi hivyo ni:

·         Enzi za kale (old age),

·         Enzi za giza ( the dark age),

·         Enzi za ufufuko (Renaissance period),

·         Enzi za kati (middle age),

·         Enzi za sasa (late age).

Historia ya tafsiri nchini Tanzania haina mda mrefu sana kwani inaanzia mnamo karne ya 19 ambayo tunaweza kugawa historian a maendeleo katika vipindi vitatu ambavyo ni: Kabla ya utawala wa kikoloni, Wakati wa utawala wa kikoloni na baada ya uhuru.

Kabla ya utawala wa kikoloni. Kaika kipindi hiki, Wamisionari walitafsiri vitabu mbalimbali vya kikristo ikiwemo Biblia takatifu kutoka lugha ya kiingereza kwenda Kiswahili na lugha nyingine za makabila kwa lengo la kueneza dini na ustaarabu wa kikristo kwa waafrika.

Wakati wa utawala wa kikoloni. Hiki ni kipindi kuanzia miaka ya 1800. Katika kipindi hiki wakoloni hasa waingereza walitafsiri maandiko mbalimbali ya kitaaluma na fasihi ya ulaya kwa lugha ya Kiswahili. mfano, Fasihi   zilizotafsiriwa ni tamthiliya ya Mzimu wa Watu wa Kaleiliyotafsiriwa na Mohamed S. Abdalla (1960) kutoka lugha ya kiingereza (Shrine of The Ancestors)

Baada ya uhuru ambayo ni kuanzia wakati 1961. Katika kipindi hiki wapo wataalamu waliofanya juhudi za kutafsiri vitabu mbalimbali kwa lugha ya Kiswahili mfano mzuri ni Mwalimu Julius K. nyerere ambaye alitafsiri vitabu viwili vya mwandishi mashuhuri wa tamthiliya wa huko Uingereza William Shakespeare ambavyo ni tamthiliya ya Julias kaizari (Julius Caesar) (1963) na tamthiliya ya Mapebari wa Venis (The Mechant of Venis) (1969). Kazi nyingine zilizotafsiriwa baada ya ukoloni ni pamoja  na kitabu cha ushairi cha Wimbo wa Lawinoiliyotafsiriwa na Paul Sozigwa (1975) kutoka lugha ya kiingereza (Song of Lawino), riwaya ya Uhuru wa Watumwa iliyotafsiriwa na East African Litertature Bureau (1967) kutoka lugha ya kiingereza (The freeing of The Slaves in East Africa). Pia  kazi nyingine za fasihi zilizotafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili hapa Tanzania ni pamoja na na Nitaolewa Nikipenda ambazo kimetafsiwa na Crement M. Kabugi (1982) kutoka lugha ya kiingereza ( I will merry When I Want).

Kwa sasa maendeleo ya tafsiri nchini Tanzania yamepiga hatua kubwa  kutokana na kukua kwa sayansi nta teknolojia. Taaluma ya tafsiri kwa sasa inafundishwa katika elimu ya sekondari na vyuo mbalimbali. Pia, taasisi na asasi zinazojishughulisha na tafsiri zimeongezeka. Kwa mfano, Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA), Taasisi ya Kiswahili na Lugha za Kigeni (TAKILUKI), Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA), Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI) na International Language Orientation Services (ILOS). Pia, wapo wafasiri mbalimbali binafsi wanaofasiri lugha wanaofasiri lugha mbalimbali kama vile Kiingereza, Kiswahili, Kiarabu, na Kifaransa.

Hivyo, Taaluma ya tafsiri inazidi kukua hadi karne kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia yanayofungamana na maendeleo ya taaluma ya lugha na ongezeko la mataifa huru yanayozungumza lugha tofauti. Kwahyo, tafsiri ni kama nyenzo kuu ya kuunganisha watu wa mataifa haya na hutumika kama njia kuu ya mawasiliano.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

                                      MAREJEO

As-Safi (1997) “Translation theories, strategies”.

Cartford, (1965). A linguistic Theory Translation.

Mshindo B.H, (2010). Kufasiri na Tafsiri. Oxford University Press. Dar es salaam.

Mwansoko na Wenzake, (2006). Kitangulizi cha Tafsiri, Nadharia na Mbinu. TUKI. Dar es salaam.

Sofer. M, (2006). The Translator’s Handbook. Schreiber Publishing Rockville. U.S.A.

Wanjala, S. F. (2011). Misingi ya Ukalimani na Tafsiri. Kwa shule, vyuo na ndaki.  Serengeti Bookshop. Mwanza.

Comments

Popular posts from this blog

My education history